-->

Mtalaamu: Kufanya mapenzi mara nyingi hupunguza tatizo la tezi dume kwa wanaume

GUSA HAPA CHINI KUPLAY VIDEO

Mtalaamu: Kufanya mapenzi mara nyingi hupunguza tatizo la tezi dume kwa wanaume

Dar es Salaam. Kama wengi wataamua kufuata usemi wa “kinga ni bora kuliko tiba”, basi waifuate huku wakichukua tahadhari dhidi ya mambo mengine. Lakini Rais wa Chama cha Wataalamu wa Matumizi ya Mionzi katika Uchunguzi na Tiba (Tara), Dk Stephen Mkoloma anasema kufanya mapenzi mara kwa mara ni moja ya njia zinazoweza kusaidia kupunguza matatizo ya tezi dume kwa wanaume. Hata hivyo, mtaalamu huyo anawaonya wanaume kutofanya tendo hilo kiholela kwa sababu ya kukwepa tezi dume, akisisitiza kuwa madhara mengine yanaweza kuwa ni kuambulia kupata magonjwa ya zinaa ukiwamo Ukimwi. 
Alisema, “Tukishauri kufanya mapenzi ya mara kwa mara fanya nyumbani kwa mke wako, kama hauna mke basi oa na ikishindikana Mungu ni wa rehema atatulinda kama wale wengine wasiofanya lakini hawajapata madhara ya tezi dume.” Akijibu maswali kutoka kwa baadhi ya wanaume waliotaka kujua ukweli kuhusu tendo hilo kama linasaidia kuwaepusha na tezi dume baada ya kujitokeza kupima katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Tawi la Mloganzila, Dk Mkoloma alisema kiuhalisia kila mwanaume ana tezi dume. 

“Ili tezi dume ifanye kazi inategemea mfumo wa homoni zinazofanya kazi sawasawa, na ili huu mfumo uwe imara unahitaji homoni ziwe vizuri na zinakuwa vizuri baada ya kupata msisimko ambao hutokea kwenye tendo la ndoa,” alisema. Hata hivyo, alisema wapo baadhi ya watu ambao hawafanyi tendo hilo kutokana na imani au sababu nyingine, lakini hawana matatizo ya tezi dume. “Baada ya kuelewa hivi isije kutuondolea ile tunu yetu ya maadili, watu waanze kurukaruka kwamba ukiona sketi unataka ooh nina tezi dume, hapana.” Dk Mkoloma alisema tezi dume si ugonjwa, isipokuwa ni kiungo katika mwili wa mwanaume. Alisema, 
“Sasa katika kuishi tezi inaweza kupata matatizo kama kansa, kuongezeka kwa ukubwa, kubadilika umbo, kwa hiyo tunachokiogopa kwa tezi dume ni isipate ugonjwa.” Alisema jambo la msingi ni kwa wanaume wenye umri wa kuanzia miaka 45 kupima ili akipata majibu kuwa ana tatizo aanze matibabu mapema. Dk Mkoloma alisema wanaume wengi wamekuwa wakijitokeza kutibiwa wakiwa kwenye hatua za mwisho za ugonjwa huo.

 “Kwa hiyo maadhimisho haya ya siku ya wataalamu wa matumizi ya mionzi na tiba tuliwalenga wanaume kwa sababu wanawake wanazo kampeni nyingi,” alisema. Hofu ya kupima Awali, Mkurugenzi wa Huduma Shirikishi Tiba, Dk Paraxeda Ogweyo alisema wanaume wengi walikuwa wanahofia kujitokeza kupima kwa kufikiria kuwa njia itakayotumika ni ile ya kutumia vidole kuing08/11/2018 Mtalaamu: Kufanya mapenzi mara nyingi hupunguza tatizo la tezi dume - Habari | Mwananchi  sehemu za haja kubwa. “Tuliona njia hiyo ya kuingizwa vidole itawakera watu, 
tumejipanga zaidi tunapima kwa mashine ya ‘ultra sound’, kwa hiyo wanaume wakisikia kampeni kama hii wajitokeze,” alisema. Dk Ogweyo alisema mwitikio wa waliojitokeza kupima ulikuwa mkubwa na kwamba, wana imani wakitangaza tena watajitokeza wanaume wengi zaidi. Akielezea kampeni hiyo, mtaalamu mwingine wa radiolojia, Lulu Sakafu alisema kansa ya tezi dume duniani ni namba mbili kwa wanaume na tatu kwa akina baba hapa nchini. Dk Sakafu alisema wanaume ambao katika koo zao wapo waliowahi kupata tatizo hilo wana uwezekano mkubwa wa kuugua, hivyo ni vizuri kupima mapema na kupata matibabu. 

“Tafiti zinaonyesha sasa hivi wanaume wa Kiafrika wanapata zaidi (tezi dume) kuliko wanaume wa maeneo mengine (duniani),” alisema. Mbali na kupima mara kwa mara, Dk Sakafu aliwashauri wanaume kufanya mazoezi ya mara kwa mara pamoja na kuacha vyakula alivyovitaja kuwa ni vya ‘kisasa’. Akizungumza baada ya kupima, Nelson Ngani alisema, “Elimu hii na wake zetu waambiwe, kwamba tendo la ndoa ni tiba siyo tu starehe, waache uvivu na visingizio vya mara kwa mara.”
Share :
Facebook Twitter Google+

Related Posts :

 
Back To Top